Thursday 2 June 2011

Uzinduzi Wa Flaviana Matata Foundation Wafana Jijini
Dar es Salaam.


Mwanamitindo Flaviana Matata anayefanya kazi zake za uanamitindo katika jiji la New York nchini Marekani.Akizungumza machache wakati wa uzinduzi wa Taasisi yake inayoitwa FLAVIANA MATATA FOUNDATION itakayokuwa ikisaidia na kusomesha watoto wa kike wasiokuwa na wazazi au walezi (Yatima).

Taasisi hiyo ambayo itakuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakisaidia jamii hapa nchini akiwemo Mbunge wa Singida Mjini Mh. Mohammed Dewji, Mwamvita Makamba pamoja na wadau wengine.

Uzinduzi huo umefanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski na kuhudhuriwa na watu mbalimbali maarufu wakiwamo Wabunge, Wafanyabiashara wakubwa pamoja na Viongozi wa Serikali.

Hongera Sana Flaviana Matata.

1 comment: